SectionsExitMajukumu Katika Familia

Majukumu Katika Familia

Wedding,Ordinary Time,Easter,Christmas,Christmas,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Lent,Easter,Marian,Christmas,Marian,Ordinary Time,Lent,Ordinary TimeExit
Chorus

Baba mama na watoto wao ni familia kamili

Na hawa wote ni muhimu, kujenga kanisa la Yesu

Katika kujenga Kanisa la Yesu ujenzi huanza nyumbani

Na kupeana majukumu, kila mmoja na lake

Chorus

Mama awe katekista, na baba awe padre

Mama awe katekista, na baba awe padren{Watoto wawe ubao[ubao] kufundishia wengine

Ili wengineo wajifunze, kuishi maisha mema} *2

Verse 3

Mama awe katekista maana yeye ndiye mwalimu[yeye],

Kwa kuwa ana huruma[sana] na ni mlezi wa watoto

Awafundishe mema yote, upendo sala na bidii[ya kazi]

Na kuwafundisha nidhamu kwa wenyewe na kwa wengine

Verse 4

Baba yeye awe padre, tena yeye ndiye mchungaji[mwema]

Ashirikiane naye mama, watoto wao kuwalea

Awe mwelekezaji pale watoto wanapopotoka [warudishwe]

Ili waweze kujenga familia iliyo bora

Verse 5

Mama awe katekista maana yeye ndiye mwalimu[yeye],

Kwa kuwa ana huruma[sana] na ni mlezi wa watoto

Awafundishe mema yote, upendo sala na bidii[ya kazi]

Na kuwafundisha nidhamu kwa wenyewe na kwa wengine

Verse 6

Watoto wawe ubao ubao, kufundishia wengine[waige]

Kwa tabia zao nzuri na uadilifu mwema

Watakuwa ni mfano bora na kielelezo sawia [cha kuigwa]

Hiyo ndiyo familia ya kumpendeza Mungu

Verse 7

Baba mama na watoto wao ni familia kamili

Na hawa wote ni muhimu, kujenga kanisa la Yesu

Katika kujenga Kanisa la Yesu ujenzi huanza nyumbani

Na kupeana majukumu, kila mmoja na lake