SectionsExitMaatumaini Ya Safari

Maatumaini Ya Safari

Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,LentExit
Verse 1

Matumaini ya safari yetu, sasa yameingia dosari

Kwani meli tuliyopanda, kuja kwako,

Tazama imevamiwa na majambazi

Hatuna njia nyingine itakayotuokoa kwenye janga hili

Yesu mwema njoo haraka, utuokoe wanao tunakwisha wote

Verse 2

Gonjwa hatari, lisilotibika, ona linatumaliza wote

Halichagui halibagui, linafyeka,

Ukimwi, halina huruma kwa wanadamu

Limeua watu wengi, ni wengi wakubwa kwa wadogo wamepotea

Milenia tuliyomaliza, ilijaa huzuni na majonzi kila upande

Verse 3

Wanasayansi madaktari, wanaahangaika kutwa kucha

Juhudi zinagonga mwamba, hakuna dawa

Ee Bwana tunakufa tuonee huruma

Tunaomba Mungu Mwenyezi, ingilia katika uwezo wako wote

Macho yao uyafumbue, fanaka ipatikane, Bwana tunakuomba

Verse 4

Tumeshaomba, tumesali sana, ee Bwana sikia sala zetu

Tunaungama tumekosa Mungu Mwenyezi,ntazama, Tunakulilia tusikilize

Tunakufa kama nzige, ee Mungu ee Bwana tunateketea wote

Si Sodoma wala Gomora, jamani hili linazidi tena latisha

Verse 5

Ee Yesu Mwema, mwenye huruma, tunakuomba ututazame

Damu na maji vilivyotoka mwilini mwako

Zilete dawa halisi ya kutuponya

Watoto ni wengi sana wanakufa bila ya hatia, inasikitisha

Wengine sasa ni yatima, hawajui wataishi vipi maisha yao

Verse 6

Tunakuomba, ee Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu

Milenia tuliyoianza, njoo Bwana,

Haraka ukatawale mioyo yetu

Machozi tunayolia yafute maovu yetu yote kwa neema yako

Lakini mapenzi yako yatimizwe vile utakavyotuashiria