Mama Maria tuambie, uliona nini njiani
Nanyi mitume tueleze mliyemkuta pangonin{ (kweli) Ni malaika, toka mbinguni
Tulimwona pale kaburini } *2
Lo! Kaburi wazi!
Hayumo, ni mzima, hayumo, amefufuka *2
Lo! Kashinda kifo!
Mauti, yameshindwa, tuimbe, tushangilie *2
Amefufuka ni hakika, amefufuka kweli kweli
Dunia nzima ifurahi, hata mbinguni wanaimban{ (kweli) Twimbe tucheze, twimbe turuke,
Twimbe sana , twimbe aleluya } *2
Nguvu za shetani kashinda, kamba za mauti amekata
Ngome ya kuzimu kavunja, kaburi za wafu zafungukan{ (kweli) Simba wa Yuda, amenguruma,
Walinzi nao mbio watimua } *2
Ameondoka kaburini, aelekea Galilaya
Nasi twendeni hima hima, twendeni kule Galilayan{ (kweli) Twendeni leo, twendeni sote,
Tumwimbie nyimbo za ushindi } *2
Tumekombolewa kwa damu, damu yake Mwanakondoo
Lango la mbingu liko wazi, kwao waliokombolewan{ (kweli) Tukimwamini, tutaingia,
Tutaishi na Mungu milele } *2