SectionsEntranceKwa Nini Wanipiga

Kwa Nini Wanipiga

Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,LentEntrance
Chorus

{ Kama nimesema vibaya toa ushahidi wa neno baya

Bali kama nimesema vema kwanini wanipiga? } *2

Verse 2

[ s ] Pilato alimhukumu Yesu, ingawa hakuona kosa kwake

Aliwaogopa Wayahudi, na kubembeleza urafiki wa Kaisari

Verse 3

Ndugu yangu tafakari kwa makini, mamlaka ulopewa na wenzio

Unayatumia ipasavyo au waumiza wenzako kama Pilato

Verse 4

Askari usalama wa raia, acheni kuwadhulumu raia,

Na kusingizia watu kesi, mnasababisha uvunjaji wa sheria

Verse 5

Mahakimu na mabingwa wa sheria, haifai kuipotosha sheria,

Maskini wajane na yatima mnawanyang`anya haki zao hukumuni

Verse 6

Waganga wakunga na wauguzi, tibuni bila kudai zawadi,

Watu masikini na yatima wanahangaika vitandani hadi kufa

Verse 7

Wanandoa tunzeni ahadi zenu, kupendana katika shida na raha,

Pia kuwalea wana katika njia impasayo Mkristo

Verse 8

Utoaji wa mimba bila sababu, na kutupa watoto majalalani,

Ni kutoujali utu wa mtu, na kuwahukumu kifo wasio na kosa

Verse 9

Dunia yetu inawaka moto, amani yetu imeshatoweka,

Vita vyatawala kila kona kisa ni tamaa ya mali na madaraka