SectionsExitKwa Jinsi Ujionavyo

Kwa Jinsi Ujionavyo

Ordinary Time,Easter,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Chorus

Kwa jinsi ujionavyo (ndivyo) ndivyo ulivyoumbwa

Tena kwa mfano wake Yesu Kristu Mwokozi wetu

Furaha leo tuimbe shangwe

Tupige ngoma filimbi na vigelegele

Tufurahi tufurahi na Bwana Yesu

Verse 2

Yeye mwenyewe aliona kwa jinsi hii utapendeza

Sasa mbona wewe wamsahau Bwana Mungu wako

Waisahau hata Sabato siku ya kumshukuru Mungu

Verse 3

Tusijiongeze vitu vingine ndugu vya kujipamba

Njoo kwake Bwana Yesu atakupamba upendeze

Ili uweze kufika kwake Mungu kwenye uzima milele

Verse 4

Ni Yesu Kristu peke yake aliye na upendo zaidi

Katuandalia karamu kabla ya mauti yake

Kaibariki kila tuilapo tupate uzima milele

Verse 5

Ulapo bila kustahili ndugu ungoje hukumu yako

Alisema mwenye moyo safi ajongee mezani

Siku ile ya hukumu nitamwita kwenye ufalme Mbingunin