(Kunapendeza kutazama kwake Bwana, nnyumba yake Bwana inapendeza) *2.
Inapendeza (kweli) inapendeza (sana),ninapendeza inafurahisha moyo.
Nyumba ya Bwana inapendeza.
(Kuna furaha kuingia kwake Bwana, nnyumba yake Bwana ina furaha) *2
Ina furaha (kweli), ina furaha (kubwa),nina furaha ni furaha ya mbinguni.
Nyumba ya Bwana ina furaha
(Kuna Baraka kuabudu kwake Bwana,nnyumba yake Bwana ina Baraka) *2
Ina Baraka (kweli) ina Baraka (nyingi),nina Baraka inayo baraka tele.
Nyumba ya Bwana ina Baraka
(Kuna chakula kutulia kwake Bwana,nnyumba yake Bwana ina chakula) *2
Ina chakula (kweli), ina chakula (kingi),nina chakula ni chakula cha roho zetu.
Nyumba ya Bwana ina chakula
(Kuna uzima kusujudu kwake Bwana,nnyumba yake Bwana ina uzima) *2
Ina uzima (kweli) ina uzima (tele), inanuzima ni uzima wa milele.
Nyumba ya Bwana ina uzima