Kivumbi
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Christmas,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Easter,Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Christmas,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1
Hapo ndipo tulipomfurahia Bwana Mungu wetu
Hirizi na mizimu yote viliposhindwa kusimama
Shetani naye kivumbi kakitimua kakimbia
Chorus
{Hapo ndipo tukasema hebu Mungu aitwe Mungu
Hapo ndipo tukasema yeye apewe sifa
Hapo ndipo tukasema atawale Mungu milele } *2
Verse 3
Tazama Bwana alipounyoosha mkono wake mkuu
Wachawi wote wakakoma, mapepo na yakanyamaza
Waganga na tunguri zao kwa aibu wakaduwaa
Verse 4
Bwana alipoinua mkono hodari kwa wagonjwa
Wakoma wakatakasika viziwi wakasikia
Viwete wakarukaruka kwa furaha wamepona
Verse 5
Jicho la Bwana lilipowaelekea watu waovu
Hasira, chuki na majivuno vyote vikatoweka
Kiburi na maringo yao hapo ndipo vikapotea