Verse 1
Kimya bara na bahari, kimya mbingu na dunia
Bwana na Muumba wenu, mtoto Yesu asinzia
Chorus
Kimya, kimya, asinzia, mpenzi wetu mtoto Yesu * 2
Verse 3
Amelazwa manyasini, mchanga mkiwa, myonge pia
Yosefu na Maria wamo, mtoto Yesu kumtunzia
Verse 4
Malaika wanashuka, mfalme wao kumlindia
Wanatunga nyimbo nzuri, mtoto Yesu kumwimbia
Verse 5
Wachungaji waja mbio, kwa mshangao waingia
Waanguka magotini, mtoto Yesu kumuabudia
Verse 6
Nasi pia twende hima, Mungu wetu kumwangalia
Twende sote kwa juhudi, mtoto Yesu kumwamkia