Mate yakamkauka, moyo ukaganda,
Na akakumbuka hali ya bustani Getsemani
Mwili wake ulipotona jasho la damu
Ngozi ikasinya, roho ikalia
Na akang'ata meno kwa maumivu makali
Kovu za misumari zilipouma upya
Maisha ya vijana wa leo, yanatonesha majeraha ya Yesu
Yale matendo yamo kwa giza, yanamliza kilio cha damu
Akatazama kwenye kwenye vijiwe
Vijana wamevuta wamelewa
Kaona nyumba za wageni
Wenyeji wanagawana ukimwi
Kwa zahanati kuna foleni
Vijana wanavinyonga vichanga
Usiku kucha, dodo mapanga
Vijana watafuta utajiri
Wengine hao barabarani
Wanauza hekalu la Roho Mungu
Kisigizio, ajira haba
Wateja wao ni wazazi wao
Na majasira wanageuza
Miili yao kufanya mabomu
Wakidanganywa ati dhawabu
Kumbe adhabu wanajitwalia
Tubuni sana salini ninyi
Jahazi lenu limeshatoboka
Ombeni yeye awahifadhi
Kwenye tundu la ubavuni mwake