Chorus
{Kama vile mwili ni mmoja nao unao viungo vingi
Tena na viungo vyote vya mwili ulonavyo ni vingin(Kweli) Ni mwili mmoja }*2n{Vinafanya kazi zote, kwa pamoja siku zote
Kwani vyote vya maana, na vizuri kwelikweli
Nasi sote Wakristu tushirikiane }*2
Verse 2
Kwa maana katika Roho, sisi sote tulibatizwa
Tulinyweshwa Roho mmoja, basi sote ni mwili mmoja
Verse 3
Kama sisi ni Wayahudi au sisi ni Wayunani
Tukiwa ndani ya Yesu hatuko tofauti kabisa
Verse 4
Miguu, mikono na macho masikio hata mapua
Na viungo vyote vya mwili vinafanya kazi kwa pamoja
Verse 5
Katika kanisa la Bwana sisi sote tuna nafasi
Tutumie nafasi zetu kwa huduma ya kanisa lake