Jipe Moyo

Marian,LentEucharist
Chorus

Jipe moyo Bwana yuko nawe, (tena)

Hakuachi kamwe kwani yeye akupenda

Hata shida zikikuandama (ndugu)

Umtegemee, Yesu atakuongoza

Verse 2

Njia imejaa giza na umande,

Huku watembea bila hata nuru wasi wasi

Hofu yakujaa woga watawala

Wasimama wima hujui pa kwenda

Ushujaa watoka wabaki upweke,

Bali yu pamoja na wewe

Verse 3

Ndugu watoweka wakuacha pweke,

Hata marafiki uliothamini watoroka

Hofu yakujaa woga watawala

Wasimama wima hujui pa kwenda

Ushujaa watoka wabaki upweke,

Bali yu pamoja na wewe

Verse 4

Kila utendacho, hakiwezekani,

Wajaribu sana kufaulu wala hauwezi

Hofu yakujaa woga watawala

Wasimama wima hujui pa kwenda

Ushujaa watoka wabaki upweke,

Bali yu pamoja na wewe