SectionsEntranceItengenezeni Njia Ya Bwana

Itengenezeni Njia Ya Bwana

AdventEntrance
Chorus

{ Itengenezeni njia ya Bwana, Bwana apite (mapito yake)

Yanyoosheni mapito ya Mungu wetu aingie } *2

Verse 2

Tazama namtuma mjumbe wangu, mbele ya uso wako,

Atakayeitengeneza njia yako,

Sauti ya mtu, aliaye nyikani nyikani inasema *2

Verse 3

Ondoka ee Yerusalemu, usimame juu

Tazama uione furaha,

Inayokujia, kutoka kwake Mungu, Mungu wako *2

Verse 4

Yajazeni yale mabonde yote yashusheni milima,

Panyosheni na pale palipopotoka

Tayarisheni njia na mapito ya Bwana aingie *2

Verse 5

Na watu wote wenye mwili, wataona wokovu,

Wataona wokovu wake Mungu wetu,

Kwa sababu yeye atakayetukujia ni mwokozi *2