SectionsEntranceImeandikwa Wapi

Imeandikwa Wapi

Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Nimefungua vitabu vyote nikapekua kurasa zote

Kulitafuta andiko hili sikuliona

Ni wapi palipohalalishwa matendo hayanmachafu sana yachafuayo jamii yetu sikupaona

Fungua macho mkristu, fungua macho

Giza nene limetanda, fungua macho

Ni wakati wa kukesha, fungua macho

Shetani katuzunguka, fungua macho

Imeandikwa wapi kwamba ushoga ni halali?

Wapi palipoandikwa rushwa ni funguo ya haki?n(tena) Imeandikwa wapi kwamba hirizi ni halali?

Wapi imehalalishwa wanaume kufunga ndoa?n(hiyo) Imeandikwa wapi, imeandikwa wapi?

Kurasa zote hakuna!

Imeandikwa wapi imeandikwa wapi?

Sheria zake Mungu!

Verse 2

Kemea Mkristu matendo hayo

Kwa sakramenti zote uyasafishe

Epukana nayo matendo hayo

Kwa sakramenti zake uyasafishe

Verse 3

Ingia katika shamba la Bwana

Mambo ya ulimwengu ni machafuko

Tembea katika shamba la Bwana

Zitende kazi zake kwa moyo safi

Verse 4

Njia zake Bwana usiziache

Ni barabara safi zenye amani.

Sheria za Bwana usiziache

Na maagizo yake ni ya Adili