Chorus
{Hodi ee Wachunga, amkeni msiwe na woga,
Amkeni upesi amkeni hima twende Bethlehem } *2nn{Tukamuone Mtoto, tumwimbie na nyimbo
Tumpigie na ngoma, aleluya leo } *2
Verse 2
Mwokozi kazaliwa, mjini mwa Daudi
Twende tumwone, tukamsujudu
Verse 3
Nyasi amelalia, jukumu la Maria
Akimtunza Mtoto, Mkombozi wetu
Verse 4
Wafalme wa dunia, wanajipangapanga
Wanafanya ghasia, juu ya Masiya
Verse 5
Tuimbe kwa furaha, na ngoma tumpigie
Kwa furaha na shangwe, tuimbe aleluya