Chorus
Hili ni fumbo la imani, Kristu alikufa
Kristu alifufuka, Kristu atarudi tena
Verse 2
Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,
Mwili na damu yake ziwe kiburudisho
Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,
Mwili na damu ni ishara ya penzi lake
Verse 3
Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana
Aishi ndani yangu na mimi ndani yake
Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,
Nitaandamana naye safarini mwake
Verse 4
Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,
Bila stahili ana hukumu ya milele
Tujitakase kabla ya kula karamuyo,
Kitubio ni sakramenti ya mapatano
Verse 5
Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,
Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa
Unijalie kukupenda na moyo wote,
Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni