SectionsEucharistHili Ni Fumbo La Imani

Hili Ni Fumbo La Imani

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Chorus

Hili ni fumbo la imani, Kristu alikufa

Kristu alifufuka, Kristu atarudi tena

Verse 2

Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,

Mwili na damu yake ziwe kiburudisho

Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,

Mwili na damu ni ishara ya penzi lake

Verse 3

Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana

Aishi ndani yangu na mimi ndani yake

Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,

Nitaandamana naye safarini mwake

Verse 4

Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,

Bila stahili ana hukumu ya milele

Tujitakase kabla ya kula karamuyo,

Kitubio ni sakramenti ya mapatano

Verse 5

Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,

Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa

Unijalie kukupenda na moyo wote,

Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni