SectionsEucharistHiki Ni Chakula Kwa Wote

Hiki Ni Chakula Kwa Wote

Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Chorus

Hiki ni chakula kwa wote wampendao

Mkate na divai ni chakula cha Roho

Wanyofu wa moyo twendeni tukampokee

Tupate uzima wa milele na milele

Verse 2

Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,

Mwili na damu yake ziwe kiburudisho

Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,

Mwili na damu ni ishara ya penzi lake

Verse 3

Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana

Aishi ndani yangu na mimi ndani yake

Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,

Nitaandamana naye safarini mwake

Verse 4

Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,

Bila stahili ana hukumu ya milele

Tujitakase kabla ya kula karamuyo,

Kitubio ni sakramenti ya mapatano

Verse 5

Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,

Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa

Unijalie kukupenda na moyo wote,

Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni