Hawa Ndiyo Wanaotapatapa
Hawa ndio wale wasiomkumbuka Mungu
Ndio wale wasiomtumaini Mungu
Wanataka maisha ya mkato pasipo kutoka jasho
Hutamani visivyo vyao viwe vyao
Tegemeo lao ni kwa waganga ambapo hupewa dumba
Ili wapate kudhulumu vya wenzao
Hawa ndio wale wanaotapatapa ovyo
Ndio wale wasiomtumaini Mungu
Kila siku ni kiguu na njia eti wasaka pesa
Hata kukumbuka kusali hawataki
Wamesahau ya kwamba Mwenyezi ndiye mgawa vyote
Na ndiye mpaji wa vyote kwa wanawe
Hawa ndio wale wanaomkufuru Mungu
Ndio wanaochezea Jina lake Mungu
Wanaishi maisha ya uzinzi pasipo kufunga ndoa
Na maisha yao hujaa machungu mengi
Wengine wanaharibu miili eti wawe warembo
Kana kwamba Mungu hakuwaumba vizuri
Hawa ndio wale wanaomdhihaki Mungu
Ndio wale wasioheshimu uhai wao
Wanatumia vibaya miili yao kwa ukahaba
Eti ili wajipatie kitu kidogo
Wengine wanavyolegeza ndoa sababu ya nyumba ndogo
Na kuziacha familia zikiteseka
Hawa ndio wale wanaompendeza Mungu
Ndio wale wanaoshika njia zake Mungu
Wale walioyatoa maisha yao kuwa sadaka
Kwa kumtumikia Mungu kwa undani
Wanaouthamini uhai wao pia na majirani zao
Wakisaidiana vyema na kupendana