SectionsExitHapa We Msafiri

Hapa We Msafiri

Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Easter,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary TimeExit
Verse 1

Hapa we msafiri simama na tazama (simama na tazama)

Nimekufa leo, kesho - ni zamu yakon(ona) ona vema nilivyowekwa humu,

Na nilivyoacha mali na jamaa

Verse 2

Nilitoka uchi tumboni mwa mamangu . . .

Narudia uchi, kati-ka tumbo la nchin(Sanda) sanda moja hilo ni vazi langu,

Wameninyang'anya hata senti moja.

Verse 3

Nifunike vema na hilo jembe lako . . .

Nalitangatanga, kati-ka ulimwengun(Basi) basi leo kiburi kimekwisha,

Kumbe dunia hii ni mti mkavu.

Verse 4

Nyumba yangu leo ni shimo udongoni . . .

Hakuna mlango, haku-na madirishan(Kita) kitanda changu na blanketi langu,

Ni udongo mzito wanielemea

Verse 5

Kifafanuacho wafu mbele ya Mungu . . .

Si cheo kikubwa, si da-raja si sifan(Mate-) matendo mema saa ya kufa kwangu,

Yatafungua mlango wa uwingu

Verse 6

Ole wangu mimi nilifanya ujinga . . .

Kwa kuambatana, na wa-tu wa dunian(Ona) ona wote leo wameniacha,

Hasa watu wale niliowapenda.

Verse 7

Unapojiona jiwazie mwenyewe . . .

Kufa siku moja, kwa wo-te ni laziman(Japo) japo sultani japo ni mtumwa,

Mungu atamwita ikiwa saa yake.

Verse 8

Nimekufa leo nilipona salama . . .

Nalijidhania, mwenye - afya mwilinin(na ma-) na mara moja nikaanguka chini

Labda huamini kwamba nali`mzima.

Verse 9

Yesu msalabani kateswa vikali mno . . .

Kwa kutukomboa, aka-mwaga damuye

Wahurumie wote wa toharani,

Mwanga wa milele uwaangazie.

Verse 10

Kwaherini wote kwaherini wapenzi . . .

Ninakwenda kwetu sita-rudi nyuman(Kwa he-) Kwaheri Baba kwaheri Mama yangu,

Mungu akipenda kwake tukutane.