SectionsExitHakuna Aliye Sawa

Hakuna Aliye Sawa

Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Easter,Ordinary Time,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

Hakuna aliye sawa naye Mungu

Aketiye mahali patakatifu pake

Anayetutendea mengi makuu ya ajabu

Basi yatupasa sote tumshukuru *2

Verse 2

Ardhi yarutubishwa na mvua zinyeshazo-

Kazi hiyo ni ya nani?

Angalieni mazao yastawi mashambani-

Kazi hiyo ni ya nani?

Verse 3

Watoto wanazaliwa na kukua nazo afya-

Kazi hiyo ni ya nani

Wazazi wapata riziki kuwahudumia-

Kazi hiyo ni ya nani

Verse 4

Safari zawa salama bila misukasuko-

Kazi hiyo ni ya nani

Tumshukuru kwa kuwa yeye ndiye mwenye haki-

Mapenzi yake yatimizwe