SectionsExitHabari Tuliyoleta

Habari Tuliyoleta

Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Easter,Ordinary TimeExit
Chorus

Je! Je! Ni nani aliyesadiki habari hii tuliyoleta

Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani

Maana alikua mbele zake kama mche kama mche mwororon(Na kama) kama mzizi katika nchi kavun{ Alidharauliwa na kukataliwa na watu

Mtu mwenye huzuni nyingi ajuaye sikitiko } *2

Verse 2

Ni kama mtu ambaye watu humficha uso

Aliyedharauliwa, hakuhesabiwa kitu

Hakika kayachukua, na masikitiko yetu,

Amejitwika huzuni, huzuni, huzuni yetu

Verse 3

Lakini tulidhania, yeye kuwa amepigwa

Ya kuwa yeye kapigwa kapigwa yeye na Mungu

Bali alijeruhiwa, yeye kwa makosa yetu

Alichubuliwa yeye, pia kwa maovu yetu

Verse 4

Adhabu amani yetu, ilikuwa juu yake,

Kwa kupigwa kwa sisi, sisi sote tumepona

Sisi ni kama kondoo, kondoo tumepotea

Tumegeukia njia, kila mtu njia yake