Chorus
{ Enyi watu wote pigeni makofi,
Enyi watu wote pigeni makofi,
Pigieni Bwana Mungu wetu,
Shangilieni kwa vigelegele } *2
Verse 2
[ s ] Enyi watu pigeni makofi, mpigieni Mungu,
Pigeni kelele kwa sauti ya shangwe
Verse 3
Kwa kuwa Bwana aliye juu, ni mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu wa dunia yoten
Verse 4
Bwana atawatiisha watu, wote wa nchi yake
Na mataifa chini ya miguu yake
Verse 5
Bwana Mungu wetu amepaa, kwa sauti ya shangwe
Amepaa kwa sauti ya baragumu
Verse 6
Enyi watu wote mwimbieni, Bwana naam imbeni
Mwimbieni mfalme na mshangilieni