Endeni Msiogope

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Easter,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Lent,Ordinary TimeBible Procession
Chorus

{ Enendeni, nendeni msiogope

Lihubiri neno duniani pote, nendeni }*2

Verse 2

Enyi wanafunzi wangu mimi nawatuma

Mataifa yote nendeni mkahubiri

Nendeni kwa moyo wote wala msiogope

Shikeni vyema shauri ninalowapa ee!

Verse 3

Enjili hii viumbe vyote visikie

Ili mapenzi ya Baba yatimilike

Nyumba, anasa na mali havina nafasi

Ondokaneni na hivyo nimewatuma ee!

Verse 4

Dhiki hatari na shida havitawaweza

Giza na hila za mwovu vitayeyuka

Elewa kwamba mimi nipo nanyi daima

Ondoeni shaka kwani sitawaacha ee!

Verse 5

Nanyi mkishatimiza niliyowamuru

Posho kupata na taji mtavalishwa

Itakuwa heri gani Mbinguni kufika

Enzi nitakayopewa kuwarithisha ee!