Chorus
Ee Mungu wangu unifundishe
Unifundishe kuwa mkarimu
Unifundishe kukutumikia kama unavyostahili
Kama unavyostahili,
Kutoa wala nisihesabu gharama
Kukubali mateso bila kunung'unika
Nitumike pasipo kutafuta pumziko
Verse 2
Nifanye kazi kwa moyo bila kutafuta ujira
Ee Mungu nisaidie nijitoe kwa kazi yako
Verse 3
Nisaidie kujua nafanya mapenzi yako
Nisije nikajikwa kwa kukosa uaminifu
Verse 4
Mimi askari wa Yesu ee Bwana uniimarishe
Nipigane hata kufa nikitetea jina lako