[ t ] Ee Mungu, mungu wangu ee Bwanan[ w ] Nitakutafuta mapema, nafsi yakuonea kiu x2n[ t ] Maanan[ w ] Maneno yako ni Roho na uzima
Wewe unayo maneno ya uzima wa milee x2
[ s ] Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yakuonea kiu, mwili wakuonea shauku,
Kwenye nchi kavu yenye uchovu,
Nchi kavu isiyo na maji.
[ t ] Ndipo nilikutazama, katika patakatifu,
Nizione nguvu zako, na utukufu wako,
Maana fadhili zako, ni njema kuliko uhai,
Nafsi yangu itakusifu.
[ a ] Ndipo nitakubariki, wakati mimi naishi,
Nikiinua mikono yangu, nitaliomba jina lako,
Kwa utajiri wa karamu, nafsi yangu imeridhika,
Kwa midomo ya kinywa changu, nitakusifu wewe.
[ b ] Wewe ni msaada wangu,
Katika uvuli wa mbawa zako, hupiga kelele kwa furaha.
Nafsi yangu hushikamana, haraka kwako Bwana,
Kwa midomo ya kinywa cha-a-ngu, nitaku-usifu wewe.