Chorus
{Ee Mungu Baba upokee sadaka
Sadaka safi isiyo na doa
Ni sadaka yake Mwanao mpenzi
Uliyependezwa naye } *2
Verse 2
Ni ajabu ya sadaka hii
Mkate kugeuka mwili wake Yesu
Na divai kugeuka damu yake
Verse 3
Ni sadaka ya agano jipya
Sadaka ya Bwana wetu Yesu Kristu
Iliyotolewa ili tuokoke
Verse 4
Mungu Baba tunakutolea
Sadaka yetu hii kama ukumbusho
Wa sadaka aliyoitoa Yesu