Chorus
Ee malkia wa mbingu Maria ufurahi aleluya
Amefufuka mkombozi amefufuka
Kwani mwanao uliyemchukua ametoka kaburini
Amefufuka mkombozi tufanye shangwe
Verse 2
Mauti ameyashinda Mwokozi amefufuka
Kuzimu ameshatoka Kristu na yuko hai
Shetani ameumbuka na dhambi imefutika
Verse 3
Ni kweli alivyosema ya kwamba angekamatwa
Ateswe mpaka kufa lakini angefufuka
Na sasa amefufuka ushindi tumeupata
Verse 4
Wakristu tuudumishe uhuru tuliopata
Kwa damu aliyomwaga Mwokozi msalabani
Tuache madhambi yetu tudumu katika neema