Verse 1
Dunia ni mti mkavu, nimeona nimeamini
Wanaosema ni wajanja sasa nao wapagawa
Chorus
Ukiuliza mashariki - sijui
Ukiuliza magharibi - sijui
Kaskazini na kusini - sijui
Hata nao pia wanasemezana - sijui
Dunia imebadilika - sijui
Na sisi tutakwenda wapi - sijuin
Hiki kiza chatikisa dunia yetu
Twaomba Baba tuonee huruma utuokoe *2
Verse 3
Mambo mengi yabadilika huku kule kwashangaza
Jibu limekuwa 'sijui' amani yatatanisha
Verse 4
Tumuombe Mwenyezi Mungu ashushe baraka zake
Ili tuishi kwa amani, dini zote zipendane
Verse 5
Twaiombea nchi yetu, Baba Mungu uilinde
Uiepushe na majanga na maradhi ya kutisha