SectionsExitDuka La Shetani

Duka La Shetani

Ordinary TimeExit
Chorus

Usipange foleni kwenye duka la shetani

Utauziwa dhambi faida yake mauti

Nenda ukajipange dukani kwa Bwana Yesu

Utapata kibali cha kuingia mbinguni

Verse 2

Enyi wavuta bangi, na madawa ya kulevya

Mbona mmejipanga katika duka la shetani

Verse 3

Na ninyi wala rushwa, makahaba na wachawi

Mbona mmejipanga katika duka la shetani

Verse 4

Duka lake shetani limejaa vitu vingi

Tena vyapendeza sana na kuuvutia moyo

Verse 5

Ramani ya mbinguni nenda kwake Yesu

Ramani ya kuzimu shetani ndiye mchoraji

Verse 6

Mnaofunga ndoa katika jinsia moja

Nanyi mmejipanga katika duka la shetani

Verse 7

Mavazi ya aibu dada zetu mwajivika

Mnaita vimini shetani anachekelea