SectionsEucharistChakula Cha Watoto

Chakula Cha Watoto

BaptismEucharist
Chorus

Si sawa kuchukua chakula cha watoto (si sawa)

Na kuwatupia mbwa chakula cha watoto (lakini)

Hata mbwa hula makombo yaangukayon(kutoka) mezani mwa Bwana wao

Nami natamani kuonja chakula hikin(ulicho) waandalia wanao

Japo sifai mimi nakusihi Bwana, uniruhusu tu *2

Verse 2

Nakutamani sana, Bwana wangu (mwema),

Kujongea karamuni,

Ijapokuwa mimi sina moyo safi,

Nina njaa nina kiu niruhusu tu

Verse 3

Nimejawa na dhambi, na uchafu (mwingi),

Na nimeoza moyoni

Mawazo mabaya na matendo maovu,

Hata naona aibu, niruhusu tu

Verse 4

Nisipokupokea, mwili wako (Bwana),

Sina uzima milele

Sasa niende wapi zaidi ya kwako,

Nisamehe nipokee niruhusu tu

Verse 5

Maana ulikuja, duniani (kwao),

Wenye dhambi kama mimi

Ulikula nao hata ukafa nao,

Na mimi nakuhitaji niruhusu tu