Verse 1
Cha kutumaini sina, ila damu yake Bwana
Sina wema wa kutosha, dhambi zangu kuziosha
Chorus
Kwake Yesu nasimama, ndiye Mwamba ni salama
Ndiye Mwamba ni salama, ndiye Mwamba ni salama n
Verse 3
Damu yake na sadaka, nategemea daima
Yote chini yakiisha, Mwokozi atanitosha
Verse 4
Njia yangu iwe ndefu, Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga, nguvu zake ndiyo nanga
Verse 5
Nikiitwa hukumuni, rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake, sina hofu mbele yake