Bwana nakupenda we Mungu wangu
Pembe ya wokovu na nguvu yangu
Wewe ndiwe mwamba na jabali langu
Nakimbilia kwako Mwokozi wangu
Bwana ndiye kinga na ngao yangu
Yeye ndiye mwamba na ngome yangu
Bwana ndiye kinga na ngao yangu
Sitaogopa nimwogope nanin{Kwa hiyo nitamwita astahili sifananiokoe na adui zangu *2
[t/b] Asifiwe Mungu aliye hai atukuzwe Mungu wokovu wangun[s/a] Asifiwe mwamba wa usalama, atukuzwe kati ya mataifan[t/b] Ampa mfalme wokovu wote, wokovu mkuu ampatian[s/a] Amfanyia fadhili masihi humjalia mteule waken[t/a] Kwa hiyo nitaliimbia sifa jina lako Mungu wangu
Kamba za kifo zilinizingira, maangamizi yalinivamia
Kamba za kuzimu zilinisonga, mitego ya kifo ilinikabili
Katika tabu nilimwita Mungu nilimlilia anisaidie
Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake alisikia
Kilio changu kilimfikia masikioni mwake
Hapo ndipo dunia ikatetemeka ilihangaika na kutikisika
Misingi ya milima ikayumbayumba Mungu alikuwa amekasirika
Moshi ulishuka puani mwake moto uvunjao kinywani mwake
Aliinamisha anga akashuka chini na wingu jeusi miguuni pake
Makaa mengi ya moto yakalipuka kutoka kwake
Mungu alinguruma kutoka mbinguni mkuu akatoa sauti yake
Alipulika giza mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka
Huko mawinguni makaa ya moto mvua ya mawe zikatokea
Alirusha umeme ukawapiga maadui zake wakatawanyika
Hapo ndipo bahari na dunia zilipoonekana
Mungu alinyoosha mkono wake kutoka juu akanichukua
Katika maji mengi alininyanyua akanitoa kwa adui zangu
Tegemeo langu ni Bwana Mungu aliniokoa na adui zangu
Walioniwinda aliwatisha aliwakemea wakapotea
Amenitoa hapo akanipeleka palipo na nafasi