SectionsExitBwana Anachunga

Bwana Anachunga

Ordinary TimeExit
Verse 1

Bwana anachunga uzima wangu,

Na malisho yake raha tele

Malisho mwake yale mabichi,

Kamwe mimi sitapungukiwa.

Chorus

Bwana ndiye kweli mchungaji mwema

Sitahitaji kitu chochote

Penye majani yale mabichi, ndipo Bwana atanilisha.

Sitahitaji, kitu chochote kitu chochote sitahitaji

Penye majani yale mabichi yale mabichi penye majani.

Verse 3

Penye maji mazuri matulivu,

Ndipo anaponiburudisha

Ananiongoza pasipo shaka

Njia nzuri, adili na nyofu.

Verse 4

Mabondeni mwa uvuli wa mauti

Ninapopita sitaogopa

Kwa maana Bwana yupo na mimi

Gongo na fimbo vyako faraja.

Verse 5

Meza waniandalia vitamu,

Nitashiba mbele ya watesi

Kichwa changu mafuta umepaka

Kikombe changu chajaa mema

Verse 6

Wema na fadhili zote za Bwana

Zimenijia mpaka milele

Ninaomba kwake mchungaji wangu

Nikae kwake hata milele.