Ndipo Musa na (wana) wa Israelinwakamwimbia Bwana wakinena
Nitamwimbia Bwana kwa kinywa changu
Kwa maana ametukuka sana
Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu
Naye amekuwa wokovu wangu
Yeye ni Mungu wangu na baba yangu nami nitamsifu
Bwana ni mtu wa vita, mtu wa vita
Bwana ndilo jina lake jina lake
Magari na jeshi lake Farao amewatupa baharini
Maakida yake wateule wamezama bahari ya shamu
Vilindi vimewafunikiza walizama vilindini kama jiwe
Bwana mkono wako wa kuume
Umepata fahari ya uwezo
Bwana mkono wako wa kuume wawatesatesa adui
Kwa wingi wa ukuu wawangusha chini wanaokuondokea
Utawaingiza Bwana na kuwapanda
Katika mlima wa urithi wako
Mahali pale ulipojifanyia Bwana ili upakae
Pale patakatifu ulipopaweka imara Bwana
Bwana kwa mikono yako
Bwana atatawala milele yoten
Ndipo Musa…..