Verse 1
Ndiyo dhamana, Yesu wangu
Hunipa furaha ya mbingu
Mrithi wa wokovu wake
Nimezawa kwa roho yake
Chorus
Habari njema, raha yangu
Yesu ndiye mwokozi wangu *2
Verse 3
Kumsalimu moyo wangu
Mara namwona raha yangu;
Aniletea malaika
Wananilinda, taokoka
Verse 4
Sina kinyume, nashukuru
Mchana kutwa huja kwangu;
Usiku kucha kuna nuru;
Mwokozi mbwangu, ndimi huru
Verse 5
Hali na mali, anitwaa!
Mara namwona anifaa
Nami nangoja kwa subira;
Akiniita nije mara