Asiregee moyowe, asitoke machozi
Akikumbuka Mungu wake, kwa yakenmakombozi, mtoa roho msalabani,nmtaka kufa mwenyewe, kwa sababunkumpendani, nani mfunga moyowe.
Bustani mle Getsemani, amwona Mungu
Baba, je mtu Mungu ana nini, nguvu zakenni haba, Bwana wangu waziona, dhambinza binadamu mwili wako umetona,nkama jasho la damu.
Salamu Rabi salamu, anena Yudanmbaya, mwenye moyo wake mgumu,nambusu pasi haya aliwaambia basi,nntakayembusu ndiye, mtwaeni na kwa upesi,
Yuda nani ni siye.
Yuda nani sio yeye, aliyetenda dhambi,
Tukimkosa Mungu Baba, kumdharaunnaye mwana, tukimsikitisha Roho, tunvipofu kama Yuda, tunatupa neema yake,nitokayo kwake Yesu.
Wote ni kupiga mbio, mitumewe pamoja,
Wamtia mikono yao, askari walokuja
Wampeleka hukumuni, aamuriwe na mtu
Atokaye uwinguni, mwanzi mkuu wa watu.
Mtume Petri amkanusha, amenena simjui
Uhodari umekwisha, machoye hainui
Pilato amwona Bwana, hakukosa ta neno
Asema sioni dhambi, lakini ni mwoga mno.
Hathubutu kumwachia, sioni nanawanmikono, mkimtaka Yesu muueni,nla mwanzi hilo neno mara askarinwamwanza, ni kupiga kelele, kumchekanna kumchokoza, mwenye mema milele