SectionsExitAsilegee Moyowe

Asilegee Moyowe

LentExit
Verse 1

Asilegee moyowe, asitokwe machozi,

Akimkumbuka Munguwe, kwa yake makombozi,

Mtoa roho msalabani, mtaka kufa mwenyewe,

Kwa sababu kumpenda ni, nani mfunga moyowe?

Verse 2

Bustani mle Getsemani, amwomba Mungu Baba,

Je mtu Mungu ana nini?, nguvu zake ni haba,

Rabbi wangu waziona, dhambi za binadamu,

Mwili wako umetona, kama jasho la damu.

Verse 3

'Salamu Rabi salamu', anena Yuda mbaya,

Mwenye moyo wake mgumu, ambusu pasi haya,

Aliwaambia 'basi, ntakayembusu ndiye,

Mtwaeni na kwa upesi', Yuda nani nisiye.

Verse 4

Yuda nani ila yeye, aliyetenda dhambi?

Akikosa kwa Munguwe, mtenda kwa hia na mbi,

Mwenye kumtendea mema, mtaka dhambi haoni,

Kwamba ni kutupa neema, kumwendea shetani.

Verse 5

Wote ni kupiga mbio, mitumewe pamoja,

Wamtia mikono yao, askari walokuja,

Wampeleka hukumuni, aamuliwe na mtu,

Ye kutoka uwinguni, Mwanzi mkuu wa watu.

Verse 6

Mtume Petri amkanusha, amenena 'simjui',

Uhodari umekwisha, machoye hainui,

Pilato amwona Rabbi, hakukosa 'ta neno,

Asema 'sioni dhambi', lakini ni mwoga mno.

Verse 7

Athubutu kumwachia, 'si hukumu' aomba,n'Mmoja nitamfungulia, Yesu au Baraba,

Wayahudi mwamtakani?', 'Baraba aachwe tu,

Yesu afe msalabani, damuye juu yetu'n

Verse 8

Pilato 'hukumu gani? simo nanawa mkono,

Mkimtaka Yesu mwueni', la mwamzi hilo neno,

Mara askari wamwanza, ni kupiga kelele,

Kumcheka na kumchokoza, mwenye mema milele.