Asante Yesu
Ingawa ni Mungu na tena ni mfalme, umejinyenyekeza kwa wadogo sisi
Ulishuka kwetu kukaa na sisi, unabaki kwetu daima katika Ekaristin
Asante Yesu (aleluya) kwa wema wako (aleluya)
Asante Yesu (aleluya) asante sana (aleluya)
Kujitoa kwetu (aleluya) ukawa chakula, asante Yesu, asante sana
Kujifanya kwetu (aleluya) kinywaji cha roho, asante Yesu, asante sana
Tulapo mkate huu wa uzima, tunapata uzima tena wa milele
Tunywapo kikombe hiki cha wokovu, twatangaza ufufuko wako uliye tukomboan
Kila nikikutafakari, nikiwaza upendo wako kwangu nasema
Asante Yesu asante,
Yote unayonitendea, asilani siwezi elezea,
Ee Yesu asante, Yesu asante
Unatufundisha upendo, tuwajali wote wakubwa pia wadogo
Asante Yesu asante
Leo hii umetukuka, ninaomba nami unijaze baraka
Asante Yesu Asante