Asante Kwa Wema
Ordinary Time,MarianThanksgiving
Verse 1
Bwana alinitendea mambo makuu
Nilipoita jina lake aliniitikia
Alinitegemeza katika taabu zangu
Chorus
{ Asante- kwa wema wako
Asante-kwa ukarimu
Asante kwa pendo lako nashukuru } * 2
Verse 3
Bwana ameniponya na magonjwa mengi
Pia amenikinga na ajali mbaya sana
Amenitoa katika mitego ya shetani
Verse 4
Nimetafakari upendo wake Bwana
Kujivika ubinadamu na kufa msalabani
Ili nikombolewe utumwani wa shetani
Verse 5
Ni mara nyingi sana nimetenda dhambi
Lakini Bwana Yesu hakunihukumu kwa dhambi
Hakuna kama Bwana yeye ni Mungu pekee
Verse 6
Wema wake Mungu wangu hauna mwisho
Ameniandalia makao baada ya kifo
Masharti yake niwe nimetii amri za Mungu
Verse 7
Enyi ndugu zangu mlio katika Kristu
Unganeni pamoja nami kumshukuru Mungu
Ni mema mengi sana yeye ametujalia