Anameremeta

Ordinary Time,MarianThanksgiving
Chorus

Anameremeta sana, anameremeta kama lulu

Hakika ni nyota ya asubuhi

Huyu ndiye yule mama, mama yake Bwana Yesu Kristu

Hakika ni mama Mama wa Mungu

Chorus

Kwa nini tusimshagilie, (tena) tukirukaruka kwa furaha(pia)

Na vigelegele tuvipige tukimshangilie mama Maria

Kwani kupitia kwake mama (huyo) ukombozi wetu umefika (kwetu)

Kwa nini tusimwite Yesu tukiegemea kwake Maria

Verse 3

Mama huyu mama gani, mama mwenye moyo safi

Mama aliyeleta nuru ya kuangaza kote

Mama anameremeta, tena anang'ara sana

Anang'ara kama lulu, lulu ya thamani kubwa

Verse 4

Watakatifu Mbinguni wanasifu Maria

Nao wanameremeta wakiitazama nuru

Mama huyu ni wa nuru, ni nuru ya ulimwengu

Tena anang'ara sana pia anaangaza

Verse 5

Maria naye Yosefu, walokuwa naye Yesu

Nao wanang'ara sana pia wanameremeta

Nasi tunaomsifu kuwa Maria ni Mama

Nasi tunang'ara sana pia tunameremeta