Amkeni wapenzi tufanye shangwen(Kweli) Hekaluni mwa Mungu wetu
Amkeni wapenzi tufanye shangwe n(Kweli) Hekaluni mwa Mungu wetun{Kwa vigelegele, na kwa makofi,
Kwa machezo pia kwa nderemo
Tumsifu Yaweh Jehova leo asubuhi} *2
Waumini wote wenye moyo safi njooni tuingie kwa Bwana
Njooni tuabudu njooni tusujudu pia tupigeni makofi
Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie
Enyi Baba njooni tusali pamoja ndani ya nyumba yake Baba
Enyi mama njoni pigeni kelele mbele za Bwana Mungu wetu
Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie
Ameumba mbingu ameumba nchi ameumba viumbe vyote,
Bahari ni yake mito na milima ahimidiwe Mungu wetu
Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie