SectionsEucharistAmini Kuna Chakula

Amini Kuna Chakula

Marian,Ordinary TimeEucharist
Chorus

Amin, amin, nawaambieni kuna chakula kinachowafaa,

Nacho chakula ndicho kile cha uzima wa milele

Verse 2

Amin kweli, nawaambieni mwanitafuta.

Si kwa sababu mlikula ule mkate.

Si kwa sababu mliziona zile Ishara.

Bali sababu mlikula mkashiba *2

Verse 3

Msikitendee kazi chakula kinachopita.

Bali, chakula kidumucho milele.

Chakula Musa alichowapa hakiwafai,

Kweli Babangu anawapa kifaacho

Verse 4

Kile chakula chenye uzima kweli ni mimi

Ajaye kwangu hataona njaa kamwe.

Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu

Hukaa kwangu nami hukaa ndani yake.

Verse 5

Hicho chakula chenye uzima kweli ni mimi.

Kilichoshuka toka mbinguni kwa Baba.

Mtu akila chakula hiki hatafariki.

Bali anao ule uzima wa milele.n

Verse 6

Kile chakula ninachotoa ni mwili wangu,

Kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.

Msipokula huu mwili wake mwana Adamu.

Hamna 'zima ndani yenu.n

Verse 7

Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu

Ana uzima, nami nitamfufua.

Na mwili wangu ndicho chakula kile cha kweli.

Na damu yangu ndicho kinywaji cha kweli

Verse 8

Na kama Baba aliye hai 'livyonituma,

Nami ni hai, ndimi hai kwa Babangu.

Na kadhalika, mwenye kunila ana uhai,

Kweli nasema atakuwa hai kwangu,