SectionsEucharistAmin Nawaambieni

Amin Nawaambieni

Eucharist
Verse 1

Amin kweli, nawaambieni mwanitafuta

Si kwa sababu mlikuka ule mkate

Si kwa sababu mliziona zile ishara

Bali kwa sababu mlikula mkashiba

Chorus

Amin, amin nawaambieni

Kuna chakula kinachowafaa

Nacho chakula ndicho kile cha

Uzima wa milele

Verse 3

Msikitendee kazi chakula kinachopita

Bali chakula kidumucho milele

Chakula musa alichowapa hakiwafai

Kweli Babangu anawapa kifaacho

Verse 4

Kile chakula chenye uzima kweli ni mimi

Ajaye kwangu hataona njaa kamwe

Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu

Hukaa kwangu name hukaa ndani yake

Verse 5

Hicho chakula chenye uzima kweli ni mimi

Kilichoshuka toa mbinguni kwa baba

Mtu akila chakula hiki hatafariki

Bali anao uzima wa milele

Verse 6

Kile chakula ninachotoa ni mwili wangu

Kwa ajili ya uzima wa ulimwengu

Msipokula huu mwili wake mwana Adamu

Hamna ‘zima ndani yenu

Verse 7

Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu

Ana uzima name nitamfufua

Na mwili wangu ndicho chakula kile chakweli

Na damu yangu ndicho kinywaji cha kweli

Verse 8

Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu

Ana uzima name nitamfufua

Na mwili wangu ndicho chakula kile chakweli

Na damu yangu ndicho kinywaji cha kweli