Amezaliwa Masiya Wetu
Amezaliwa Masiha wetu, hoyee hoye hoye hoye
Mwana wa Mungu mkombozi wetu, hoyee hoye hoye
Leo kazaliwa naye Maria na amelazwa
Kwenye hori la wanyama, twende tukamwone
Amekuja kwetu mwana wa Mungu kuzichukua dhambi zetu wanadamu, mkombozi wetun{ Tumsujudie Bwana Mungu,kwa vigelegele
Tucheze ngoma na kayamba tupige makofi }*2
Amelala manyasini, twendeni tukamwone,
Tukamsalimie Mkombozi wetu
Kwa zawadi zetu za dhahabu uvumba na manemane
Wachungaji waondoka, waenda Bathlehemu,
Wakamsujudie Bwana Mkombozi,
Wafurahi naye pamoja na Maria naye Yusufu
Malaika wamefika wengi na wa mbinguni
Tukajiunge nao tuimbe pamoja utukufu uwe
Kwa Mungu juu amani kwa watu wenye mapenzi mema
Tumpokee mkombozi Masiha amekuja
Ewe mtoto Yesu ishi ndani yetu, tuangaze sisi,
Kwa mwanga wako mwanga wa Mbinguni