Ameenea

Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1

// utangulizi //n

Sijaona (tena) sijaona (miye) aliye mwema kama hivi

Amejaa (tele) amejaa (huyu) huruma neema na faraja

Hanyamazi (kamwe) hanyamazi (yeye) tunapomwita huitikan(Naye) amekuwa (kwetu) ni mwaminifu tena mkweli mpaji

Chorus

// kiitikio //

Na kila kitu tunachomuomba Mungu, Yeye anatujibu

Na kila jambo tunalomuomba Bwana, Yeye anatujibu

Na kila mara tukisemezana naye, Yeye anatujibu

Na kila jambo tunalomuomba sisi, Yeye anatujibu

Na tena hashindwi jambo na hamtupi mtu

Yeye hashindwi jambo na hamtupi mtu

Verse 3

n// mashairi //

Yote mahitaji yetu, tunaomba anatupa

Hata tusiyoyajua, nayo anateremsha

Wa ajabu, ha ha nashindwa nieleze vipi

Verse 4

Mambo yakiwa magumu, ujasiri anatupa

Tunayabeba vilivyo, te na kwa uvumilivu,

Wa ajabu, ha ha kwa kweli ananishangazan

Verse 5

Siku ya kija manono, atupa uadilifu

Tupokee kwa uchaji, yeye awe mtukufu

Wa ajabu, ha ha ajabu ni ajabu tupu

Verse 6

// hitimisho //n

Heri na neema ndiye anatoa

Nguvu na uzima anatujalia

Nayo mafanikio he anatoa yeye

Kupata watoto (wazuri) ni neema zake (siyo ujanja)

Kupata elimu (ya juu) ni baraka zake (siyo akili)

Verse 7

Yupo kila mahali Mungu ameenea

Pote anasikia sana akiitwa anaitika

Yupo kila mahali Mungu ameenea

Pote kweenye mitego mikuu hata mapito ya kutisha

Yupo kila mahali Mungu ameenea

Yote tunayoyajua na tusiyoyatambua

Yupo kila mahali Mungu ameenea

Verse 8

Yupo kila mahali tu, yupo kila mahali tu

Yupo kila mahali Mungu ameenea

Ameenea ameenea, ameenea, ameenea

Ameenea ameenea, ameenea, ameenea

Kila mahali ni yeye Mungu ameenea