SectionsBible ProcessionAlidharauliwa Na Kukataliwa

Alidharauliwa Na Kukataliwa

LentBible Procession
Chorus

Alidharauliwa na kukataliwa kukataliwa na watu

Mtu mwenye huzuni nyingi ajuaye sikitiko

Verse 2

Alikua mbele zake kama mche mwororo,

Na kama mzizi katika nchi kavu,

Hakuwa na umbo kuvutia wala uzuri

Hata tumwonapo tumtamani

Ni kama mtu ambaye watu humficha uso,

Wala hatukumhesabia kuwa kitu

Verse 3

Hakika amechukua masikitiko yetu,

Amejitwika huzuni zetu amejitwika.

Lakini na sisi tulidhani kuwa kapigwa,

Amepigwa na Mungu na kuteswa

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,

Alichubuliwa kwa maovu yetu

Verse 4

Adhabu ya amani yetu ilikuwa kwake,

Na kwa kupigwa kwake yeye sisi tumepona

Sisi sote kama ko-ndoo tumepote

Kila mmoja njia yake yeye,

Bwana ameweka juu yake maovu yetu,

Alione-wa laikini alinyenyekea

Verse 5

Alionewa lakini hakufunua kinywa,

Kama mwanakondoo akipelekwa machinjio

Kwa kuonewa kuhukumiwa kaondolewa,

Ni nani atasimulia haya?

Ni nani aliyesadiki habari hii?

Na mkono wa Bwana amefunuiwa nani?