SectionsEucharistAleluya Tumwabudu Yesu

Aleluya Tumwabudu Yesu

Ordinary TimeEucharist
Verse 1

Aleluya tumwabudu Yesu Kristu

Yu hai mzima katika ekaristi

Aleluya aleluya aleluya

Verse 2

Sakramenti kuu hii ya mapendo,

Ulimojiweka kwa ajili ya watu,

Nasi twakupa yetu leo mapendo.

Verse 3

Ni sadaka ya msalaba twaijua,

Kafufuka kisha kapaa kwa Baba,

Yuko nasi katika hii Ekaristi.

Verse 4

Ni chakula chetu bora na kwa roho,

Ni Mwanakondoo yule wa pasaka,

Atulisha, atushibisha daima.

Verse 5

Njoni wote tumwabudu Yesu Kristu,

Nyoyo zetu, nyimbo zetu tumtolee,

Sifa zetu, shangwe zetu tumpatie.

Verse 6

Mwili wako uwe asili ya heri,

Utakase nyoyo zetu kwa damuyo,

Zifike mbinguni daima milele.n