Ahadi
Ordinary TimeBible Procession
Verse 1
Niliyafumbua macho yangu na kutazama,
Ili nimuone ashukapo toka winguni,
Maana aliniahidi kuwa atarudi,
Kunichukua tukafurahi pamoja naye Mbinguni
Chorus
Ilikua hamu ya moyo wangu tazama
Na bado ninatamani kipi kitanizuia
Niuone uso wa Bwana na Mungu wangu
Nimuone akitimiza ahadi yake
Verse 3
Kaniahidi nikivumilia mpaka mwisho
Nitamuona katika kiti cha enzi
Akanionya nijitenge mbali na wazushi
Wasije wakaipotosha imani yangu, hakika
Verse 4
Nijapoanguka katika dhambi ya mauti
Ataiosha ikawa nyeupe kama suti
Na tena nikimlilia katika ukunga
Atanipa uzao kama nyota za mbinguni, ajabu
Verse 5
Kwa hiyo moyo wangu umetulia kabisa
Kwa kuwa nimejua kwamba ipo tumaini
Atukuzwe Baba Mwana na Roho Mtakatifu
Kama ilivyo mwanzo, sasa na mileleyote amina