SectionsEntranceAcheni Ninyi Acheni Kabisa

Acheni Ninyi Acheni Kabisa

Marian,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Acheni ninyi, acheni kabisa, acheni kuwapendelea waovu

Wateteeni wanyonge na yatima, wapeni haki masikini na fukara

Waokoeni wanyonge na maskini katika makucha ya wadhalimu

Verse 2

Acheni kutoa hukumu, hukumu isiyo ya haki kwa wanyongen{Kwa kuwa (kwa kuwa) wanyonge na maskini ni wa Mungu

Msiwakandamize wanyonge kwa kuwatetea waovu } * 2

Verse 3

Lakini ninyi hamjui, aliyewapa mamlaka ni nani

Ni yeye (ni yeye) anaye uchukia uovu

Anayeuchukia uovu na kuwapenda maskini

Verse 4

Maisha ya dunia ni mafupi sana ndugu kumbukeni

Na ninyi (na ninyi) mtakufa kama wakuu wengine

Kama walivyokufa na kuyaacha madaraka na mali