Chorus
Acheni ninyi, acheni kabisa, acheni kuwapendelea waovu
Wateteeni wanyonge na yatima, wapeni haki masikini na fukara
Waokoeni wanyonge na maskini katika makucha ya wadhalimu
Verse 2
Acheni kutoa hukumu, hukumu isiyo ya haki kwa wanyongen{Kwa kuwa (kwa kuwa) wanyonge na maskini ni wa Mungu
Msiwakandamize wanyonge kwa kuwatetea waovu } * 2
Verse 3
Lakini ninyi hamjui, aliyewapa mamlaka ni nani
Ni yeye (ni yeye) anaye uchukia uovu
Anayeuchukia uovu na kuwapenda maskini
Verse 4
Maisha ya dunia ni mafupi sana ndugu kumbukeni
Na ninyi (na ninyi) mtakufa kama wakuu wengine
Kama walivyokufa na kuyaacha madaraka na mali