SectionsEntranceAcheni Mimi

Acheni Mimi

Ordinary TimeEntrance
Chorus

{Acheni mimi, nimuimbie muumba wangu,

Aliyeniumba, mimi kiumbe mwenye akili}*2

Aliyenipa uwezo wa kusimama hapa

Tangu tumboni mwa mama amenipa uhai

Juzi jana leo nimeamka kesho ajua yeye

Maisha yangu ayapa maziwa ni kama mtoton{Acheni mimi, nizitamke sifa za Mungu wangu

Na sitachoka, kumuimbia mimi ningali hai}*2

Verse 2

Nalala jioni na kuamka pia nazo nguvu,

Ninafanya kazi na kujipatia riziki zangu

Verse 3

Amenipatia akili yangu na wangu ubunifu,

Shuleni kazini ninayoyafanya hayana pungufu

Verse 4

Mara nyingi sana ninajiuliza nitampa nini,

Kwani Bwana amenitendea mengi bila ya kwa nini

Verse 5

Ninapokuwa nazo shida nyingi hunipa tulizo,

Kwake kila mara watu wote hupata burudiko.