Acheni Kukata Tamaa
{Mwenyezi ameniumba, akanileta kati yenu, Niwakumbushe watu wake thamani yenu duniani}*2n{Acheni acheni kufa moyo, Acheni acheni kukata tamaa, Yeye aliyewaumba anaijua kazi yake}*2
Aliijua siri yenu hata kabla hamjaumbwa,
Ramani ya maisha yenu, yote imo mikononi mwake
Magonjwa yanayowatesa na maumivu yasiyokoma,
Ni madogo kuliko yale aliyoyaponya kwa sekunde
Hali mbaya ya kiuchumi, mlo mmoja madeni mengi
Ni njia ya kunyenyekea na kumpa Mungu mkuu
Misiba inayowaliza mnapofiwa na ndugu zenu,
Ni njia ya wapendwa wenu kwenda mbinguni wakafurahi
Maumivu ya kuonewa kudhulumiwa kusingiziwa
Ni nafasi ya kusamehe na kujivika utakatifu
Matatizo ya ndoa zenu na migogoro ya familia,
Ni bahati mmejaliwa ya kujifunza uvumilivu
Bebeni misalaba yenu, nyamazeni msinung'unike
Huo ndio wokovu wenu shikilieni msiachie